Ticker

7/recent/ticker-posts

‘HELA ZA MAGOLI YA SIMBA, YANGA BADO ZIPO’

  

Nembo ya Yanga

“Kwa sasa hivi niwahakikishie wale waliokuwa wakitania jana, niliona utani nampigia Msigwa namwambia ‘ebu maliza mpira haraka mimi pesa zimeisha’, nataka niwahakikishie kwamba Mama bado anazo wekeni mipira kwenye wavu jengeni jina la Nchi yetu, bado zipo,”amesema Rais Dkt. Samia.

 

Rais wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan amesema bado zile milioni tanotano za kununua magoli ya Simba na Yanga kwenye mechi za kimataifa zipo, ameyasema  leo akiwa Dar es salaam katika Sherehe za maadhimisho ya miaka miwili ya Serikali ya awamu ya sita iliyoandaliwa na Umoja wa Wanawake wa CCM (UWT). 


Mchezaji wa simba, Chama
“Niwapongeze Wanangu wa Yanga na Simba kwa kuitumia vizuri fursa niliyowapa ya goli moja milioni 5 wameitumia vizuri sana, kwa hesabu nilizonazo nadhani Yanga wameshalamba milioni 30 na Simba jana milioni 35 na nyuma nadhani walikula 5 kwahiyo niwapongeze kwa kuitumia vema fursa hii, niwapongeze na ni imani yangu kwamba ile kasi iliyopo miguuni ya milionk tano kwa goli itaendelea kuwepo huko mbele milioni tano zitakapoondoka”

 

“...niliona utani nampigia Msigwa hembu maliza mpira haraka mimi pesa zimeisha, nataka niwahakikishie kwamba mama bado anazo, wekeni mipira kwenye wavu, jengeni jina la nchi yetu".

Post a Comment

0 Comments