Ticker

7/recent/ticker-posts

LUCY NA LIANA WAPELEKWA SONGEA KUCHOCHEA UTALII WA SIMBA

SERIKALI kupitia Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania (TAWA) chini ya Wizara ya Maliasili na Utalii  imeleta  Simba wawili majike wanaoitwa Lucy na Liana katika bustani ya wanyamapori ya Ruhila iliyopo Manispaa ya Songea  mkoani Ruvuma ili kuchochea utalii wa ndani

Akizungumza kwenye hafla ya upokeaji wa Simba hao iliyofanyika ndani ya bustani ya Ruhila mjini Songea, Mkuu wa Utalii kutoka Mamlaka ya Usimamizi wa  Wanyamapori Tanzania (TAWA) Kanda ya Kusini Mashariki Kamishina Msaidizi Said Mshana  amesema Simba hao wametoka hifadhi ya wanyamapori  ya  Sevo jijini Arusha.

Post a Comment

0 Comments