![]() |
| James Chuyi, Afisa Mazingira , Ofisi ya Makamu wa Rais |
Serikali ya Tanzania imeeleza dhamira yake ya kuimarisha mikakati ya kitaifa na kikanda ya kukabiliana na changamoto za mabadiliko ya tabianchi, uharibifu wa mazingira na uhamiaji wa watu unaochochewa na athari za hali ya hewa.
Kauli hiyo imetolewa hivi karibuni na James Chuyi, Afisa
Mazingira kutoka Ofisi ya Makamu wa Rais, katika Mdahalo wa Kitaifa kuhusu
Utekelezaji wa Azimio la Mawaziri wa Kampala kuhusu Uhamiaji, Mazingira na
Mabadiliko ya Tabianchi. Chuyi alisema Tanzania inakabiliwa na athari kubwa za
mabadiliko ya tabianchi ikiwemo mafuriko ya mara kwa mara, ukame wa muda mrefu,
na kuongezeka kwa viwango vya maji ya bahari. Matukio haya yamesababisha
uharibifu wa miundombinu, kupungua kwa uzalishaji wa kilimo na kuwalazimisha
maelfu ya wananchi kuhama makazi yao. “Athari hizi si masuala ya kimazingira pekee bali pia ni
changamoto za kibinadamu na maendeleo zinazogusa kiini cha jamii yetu,” alisema
Chuyi. Alisema kwa mwaka 2004 pekee, watu zaidi ya 278,000
waliathirika na mafuriko, huku ukame ukiathiri mfumo wa chakula na uchumi.
Chuyi alisisitiza kuwa mpango wa kitaifa wa utekelezaji wa Azimio la Kampala (KDMECC)
utasaidia kuunganisha juhudi za kitaifa na za kikanda. Kuhusu mikakati na ushirikiano wa kikanda, Azimio la
Mawaziri wa Kampala, lililoidhinishwa Julai 2002 na kusainiwa na Tanzania mnamo
2022, linahimiza ushirikiano wa kikanda katika kushughulikia changamoto za
tabianchi na uhamiaji. Tanzania kwa sasa ipo kwenye hatua ya kuandaa Mpango wa
Kitaifa wa Utekelezaji, sambamba na utekelezaji wa Mkakati wa Kitaifa wa
Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi unaotarajiwa kukamilika 2026. Maurizio Busatti, Mwakilishi Mkazi wa Shirika la Kimataifa la Uhamiaji (IOM) nchini Naye Maurizio Busatti, Mwakilishi Mkazi wa Shirika la
Kimataifa la Uhamiaji (IOM) nchini, alisema kuwa uhamiaji umekuwa njia ya
binadamu kukabiliana na majanga kwa karne nyingi. Alisisitiza kuwa ni muhimu
kulinganisha changamoto na fursa za kikanda na utekelezaji katika ngazi ya
kitaifa na za mitaa. Aliongeza kuwa changamoto zinazoikabili Tanzania ni pamoja
na kuongezeka kwa Viwango vya Maji ya Bahari, Maziwa na Mito hivyo kutishia
makazi ya watu na shughuli za kiuchumi. Changamoto nyingine ni mafuriko mara kwa mara ambayo yanaharibu
miundombinu na mashamba, uUkame wa muda mrefu ambao unapunguza uzalishaji wa
kilimo na kuathiri usalama wa chakula pamoja na uhamiaji wa ndani unaowafanya wananchi
kuhama kutoka maeneo yenye changamoto kubwa za tabianchi kwenda mijini au
maeneo salama zaidi na hivyo kuongeza shinikizo katika miji. Upendo Mwakyusa, mwakilishi wa Asasi za Kiraia (CSOs)
Akizungumzia mchango wa asasi za kiraia, Upendo Mwakyusa,
mwakilishi wa Asasi za Kiraia (CSOs), alisema mashirika ya kiraia nchini
yamekuwa mstari wa mbele kusaidia jamii zinazokabiliwa na athari za mabadiliko
ya tabianchi. “Asasi za kiraia zinahamasisha jamii kuhusu mabadiliko ya
tabianchi, kushughulikia migogoro ya ardhi, utetezi wa sera na uhamasishaji wa
jamii, kutoa elimu ya kilimo kinachohimili mabadiliko ya tabianchi, kuhamasisha
matumizi ya nishati safi na kusaidia wahanga wa majanga,” alsimea Mwakyusa Alisisitiza kuwa wakulima na wafugaji kutoka maeneo kame,
hasa Kanda ya Kati na Kaskazini, wamekuwa wakihamia maeneo yenye mvua za
kutosha kama Kigoma na Katavi kutokana na ukame na uharibifu wa ardhi. Pamoja na hilo, Mwakyusa ameseMashirika kama ForumCC, Haki
Ardhi, Pastoral Women’s Council, na Cove Environmental Conservation yamekuwa
yakilinda maslahi ya makundi yaliyo hatarini, hasa wanawake na wasichana. Sikhulile Dhlamini, Mratibu wa Programu wa IOM Tanzania akiongea wakati wa majadiliano
Kwa upande wake Sikhulile Dhlamini, Mratibu wa Programu wa
IOM Tanzania, aliipongeza mapendekezo yaliyotolewa kupitia mashauriano na wadau
yaliyofanyika Augosti 5-6, 2025 jijini Dar es Salaam na akaahidi kuendeleza
ushirikiano na Serikali. Pia alisisitiza umuhimu wa kushirikisha vijana katika
utekelezaji wa miradi ya mazingira na tabianchi. Kimsingi, Tanzania inaelekea kwenye hatua muhimu ya
utekelezaji wa Azimio la Kampala na mikakati ya kitaifa ya tabianchi.
Ushirikiano wa karibu kati ya Serikali, mashirika ya kimataifa, asasi za
kiraia, sekta binafsi, na jamii ni msingi wa kuhakikisha kuwa changamoto hizi
zinazohusisha mazingira na uhamiaji zinatatuliwa kwa njia endelevu, ili kulinda
ustawi wa vizazi vya sasa na vijavyo. |




0 Comments