Ticker

7/recent/ticker-posts

WAKUSANYA TAARIFA WANAPASWA KUJISAJILI PDCP

 


NA MWANDISHI WETU-MOROGORO

Mkurugenzi wa Tume ya Ulinzi wa Taarifa Binafsi (PDPC), Dkt. Emmanuel Mkilia amesema kila mtu, taasisi ama Ofisi ya Umma ama binafsi inayojihusisha na ukusanyaji na uchakataji wa taarifa, inapaswa kujisajili kwenye tume hiyo.

 

Amesema, kwa mujibu wa  kifungu cha 14 cha Sheria ya Ulinzi wa Taarifa Binafsi  nchini, kutojisajili ni kosa.

Dkt. Mkilia ametoa kauli hiyo kwenye kikao cha PDPC  na Wahariri wa vyombo vya habari Machi 1,2025, mkoani Morogoro.

 

Amesema, PDPC iliyozinduliwa Aprili 3, 2024, kwa lengo la kumlinda mwenye taarifa, kusimamia sheria ya ulinzi na kufanya uchunguzi wa ukiukwaji wa haki za faragha.

 

Post a Comment

0 Comments