Ticker

7/recent/ticker-posts

LIGI KUU MSIMU HUU NI YA KIBABE

NA ELIAS SHADRACK
Michezo miwili ya ligi kuu ya NBC iliyochezwa Februri 16,2024 imekamilisha mzunguko wa kwanza wa Ligi Kuu ya NBC kwa kila timu kucheza michezo 15. Timu ya Kagera Sugar ilikuwa nyumbani kuwaalika Mashujaa Fc katika dimba la Kaitaba na Azam Fc iliwakaribisha Geita Gold katika uwanja wa Azam complex.

Kabla ya michezo hiyo ya Februari 16, Yanga ambao ndio vinara wa Ligi Kuu walikuwa wamejikusanyia alama 40 ambazo ni mara mbili zaida ya alama walizokuwa nazo mzunguko wa kwanza katika msimu uliopita. 

Pamoja na mambo mengine msimu huu umeoneka kuwa ni wa kitofauti kutokana na ushindani wa ubingwa kuhusisha timu tatu za Yanga, Simba na Azam, tofuti na ilivyozoeleka awali ambapo washindani zaidi ni Simba na Yanga.


Ni miezi mitatu tu sasa imesalia kwa Ligi Kuu msimu wa 2023/24 kukamilika hadi sasa ni ngumu kutabiri nani atakuwa bingwa.

Hadi kufikia mwishoni mwa mwezi Machi angalau wabashiri wa soka wanaweza kupata mwanga wan ani anaweza kuwa bingwa, ikumbukwe kuwa raundi ya pili ya ligi kuu iimeshaanza tangu Februari 17, 2024.

Post a Comment

0 Comments