Ticker

7/recent/ticker-posts

WAFANYABIASHARA QATAR KUWEKEZA ZANZIBAR

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Hussein Ali Mwinyi amesema ziara yake   hivi karibuni nchini Qatar alimwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Dkt Samia Suluhu Hassan kwenye Mkutano wa Jukwaa la Kimataifa la tatu la Uchumi Qatar lililofanyika jijini Doha.

Ameyasema hayo leo tarehe 30 Mei 2023 katika mkutano wake  wa kila mwisho wa Mwezi na Waandishi wa Habari   uliofanyika Ikulu, Zanzibar. 

Dk.Mwinyi amesema alipata fursa ya kueleza maeneo ya uwekezaji na biashara yanayopatikana Zanzibar  katika ziara hiyo alipokutana na Wawekezaji Nchini humo.


Aidha Dk.Mwinyi amezungumzia  sera ya Uchumi wa Buluu ikiwemo  Mafuta na Gesi , Uvuvi, Bandari , usindikaji wa bidhaa za bahari na fursa zinazopatikana  katika maeneo ya sekta ya utalii ikiwemo wa fukwe, mambo ya Kale na utalii wa kisasa wa kumbi za  Mikutano ya Kimataifa.

Vilevile  muda mchache ujao   Zanzibar itapokea  timu ya wataalamu na Wawekezaji kutoka Qatar. 


Post a Comment

0 Comments