Ticker

7/recent/ticker-posts

SAUTI SOL LASAMBARATIKA RASMI, SASA KUFANYA MATAMASHA YA KUWAAGA MASHABIKI WAO

Kundi maarufu la muziki wa Afro- pop la  Sauti Sol   lenye maskani yake nchini   Kenya sasa limevunjuka rasmi. Tangazo la kuvunjika kwa kundi hilo limetolewa jana Jumamosi, Mei 20, 2023.

Aliyetoa taarifa hiyo ni Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano cha kundi hilo, Faarah Nur.

Hata hivyo sababu za kusambaratika kwa kundi hilo hazijawekwa wazi.  Katika taarifa hiyo iliyosambazwa  kwa  vyombo vya habari, walisema kwa kifupi: “Ziara inayokuja ya Marekani, Ulaya na Kanada ni fursa kwa mashabiki kutuona  Sauti Sol kwa mara ya mwisho.

Kila onyesho litajazwa na hisia za upendo na shukrani huku bendi ikitumbuiza vibao vya milele na nyimbo zinazopendwa na mashabiki ambazo zimeacha alama isiyofutika kwenye kumbukumbu zetu za pamoja." , walisema wanachama wa kundi hilo.

Sauti Sol liliundwa mwaka 2005 likiunganisha vijana  wanne machachari watatu wakiwa waimbani na  muungano wa Moja mpiga gitaa.

Vijana hao ni  Bien-Aimé Baraza, Willis Chimano na Savara Mudigi ambao walikuwa ni waimbani na  mpiga gitaa alikuwa ni Polycarpe Otieno.


Kundi hilo lilitoa albamu yake ya kwanza mwaka 2008 iliyojulikana kwa jina la  Mwanzo.

Albamu ya pili walitoa mwaka 2011 ikiwa na jina la Sol Filosofia. Mwaka 2015 waliachia albamu ya tatu iliyobeba jina la Live and Die in Afrika na mwaka 2020 kundi lilirejea na albamu ya nne na ya mwisho.

Kundi hili lilionesha ubora mkubwa kuanzia kutunga wimbo, kutengeneza na kuimba kwa pamoja. 

Hili lilikua miongoni mwa makundi bora barani Afrika ma duniani kwa ujumla

Post a Comment

0 Comments