Ticker

7/recent/ticker-posts

MWALIMU ALIYEMNG'OA MENO MKEWE ASAKWA

Jeshi la polisi jijini Arusha, linamsaka Isaac Mnyangi (40) ambae ni mwalimu na mfanyabiashara na pia ni mjumbe wa mkutano mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Arusha kwa kosa la kumshambulia na kumdhuru mwili mke wake Jackline Mnkonyi.

Mnyangi alimto boa mke wake jicho kwa bisibisi na kumng'oa meno kwa plaizi.

Mtuhumiwa huyo anatafutwa kwa RB NO: ARS/RB/5416/2023.


Mnyangi alimshambulia mkewe Jackline Mnkonyi mwenye umri wa miaka 38 mkazi wa Sombetini Jijini Arusha Mei 23 mwaka huu majira ya saa tano usiku.

Alimpiga kipigo kikali  ikiwa ni pamoja na kumngoa meno mawili na kutobolewa jicho kwa kile kinachodaiwa kuwa ni wivu wa mapenzi.

Akizungumza na waandishi wa habari nyumbani kwa wazazi wake eneo la Sinoni kata ya Daraja Mbili Jijini Arusha,Jackline alisema kuwa baada ya kupata kipigo hicho alichukuliwa bila kujitambuwa na kupelekwa nyumbani kwa wazazi wake Sinoni na kutupwa getini bila ya kujitambua

Alisema Mume wake mara baada ya kufika eneo la nyumbani aliwapigia simu wazazi wake na wazazi wake walipofungua geti walimkuta katika hali mbaya na baadae waliamua kumchukua na kumpeleka hospital ya kaloleni kwa matibabu zaidi.


Akizungumza Mkasa huo alisema kuwa,mchana wa mei 23 mwaka huu alitembelewa na mjomba wake ambaye ni Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi(CCM) Simiyu aliyetambuliwa kwa jina la Vicent Matai .

Jackline alisema na kumtaja mume wake kwa jina la ,Isaack Mnyagi Mwalimu na mkazi wa wilayani Rombo Mkoani Kilimanjaro huja baada ya muda wa zaidi ya miezi mitatu na zaidi kuona watoto wawili aliozaa nao na siku hiyo alikuja usiku ghafla.

Alisema alipofika nyumbani Sombetini maajira ya saa 4.45 usiku aligonga mlango na kufunguliwa na watoto lakini hakutaka salamu na kuingia chumbani na alipomfuata alitoka chumbani.

Jackline alipoona hivyo alimuuliza kulikoni alichoambulia ni maneno mazito na matusi na kuulizwa mchana alikuwa na nani na alimjibu kuwa alikuwa na mjomba wake hatua ambayo alikana na kusema kuwa ni mtu wake na huwa wanafanya umalaya hatua ambayo alipinga lakini alijikutaja akipigwa na mjeledi mgongoni.

Alisema alijitahidi sana kujieleza lakini ilishindikana na Mume wake Mnyagi alichukua Plaizi kifaa cha gereji na kumwamuru afungue mdomo na kungolewa jino moja baada ya lingine huku akipata kipigo kikali na kujikuta na maumivu makali hadi jana.


Jackline alisema hatua hiyo aliona kama haitoshi aliamua kuchukua kitu chenye Icha kali na kumtoboa jicho moja ambalo hadi sasa hawezi kuona na kumwambia maneno mazito na mtusi huku akiendelea kupigwa hali iliyomfanya kupoteza fahamu.

Alisema hakujua jinsi alivyofikishwa nyumbani kwa wazazi wake Sinoni Daraja mbili na kutupwa getini kwani nilishtuka nikiwa hospital .

Nimetobolewa jicho na nimengolewa meno mawili kwa chombo kinachoitwa Plaiz nina maamuvi makali sana naiomba serikali ichukue hatua dhidi ya mume wake kwani amenifanyia unyama wa hali ya juualisema Jackline

Naye Mzazi wa Jackline,Mzee Elimilis John Mkonyi alisema kuwa baada ya kumpeleka katika hospital ya Rufaa ya Mount Meru na kupata matibabu alikwenda kituo kikuu cha polisi Arusha na kufungua jalada shambuli la kuzulu mwili kesi amba ARS/RB5416202

Post a Comment

0 Comments