Ticker

7/recent/ticker-posts

ABROMOVICH AKATAA MVINYO MUNICH

Ameandika @swaleh_shrimp.

Tajiri Abramovic anakataa Waini kutoka kwa mhudumu pale VIP na kumwambia " sikuja Munich kwa lengo la  kulewa nimekuja kushuhudia mafanikio makubwa ya klabu yangu"

Uwanja ulikuwa umeshainama Sehemu moja, mpira ni Kama vile  umeshatolewa pumzi  Bayern walishapiga Kona zaidi  ya 15, walishalijaribu lango The  blues zaidi ya mara 19.

Wakati The Bavarians  wanamkimbilia Muller kushangilia goli lake la kichwa dakika ya 83 , Frank Lampard alimuita Young Ryan Betrand na kumwambia "unawaona wale, wamesafiri zaidi ya kilometa 908  waliofika hapa kutoka London hatuwezi kupoteza kwasababu yao." Alimueleza akimuonyesha mashabiki wa Chelsea waliokuwa jukwaani wakimwaga machozi.

Bayern Munich  wakiamini shughuli imeisha, Chelsea wanafuta maji tu kibanda umiza Cha  Huku nyumbani kusini watu wanainuka na kujikunuta vumbi kwa kusema mchezo umekwisha. 

Dakika 88 inapatikana kona ya kwanza kwa Chelsea Juan Mata aliusafirisha mpira hewani na kumkuta Didier hapo ndipo  Bwana Alison Bender alisikika akilalamika kwenye kipaza sauti kwa kusema "Ni Didier Drogba labda na mpira wake wa mwisho kupiga kwa Chelsea, Drogba aliyefunga bao la nyumbani dhidi ya Barcelona, Drogba aliyesawazisha hapa Allianz Arena. It's Drogba against Manuel Neur.. Drogbaaa.."


kiniuliza leo kuhusu  ubora wa Peter Cech  nitakwambia turudi Munich 2012 mikono yake ilifuta penalt ya Robben katika dakika 30 za nyongeza. Naam alikuwa ni Peter Cech aliyeifuta penalt ya Ivica Olic. Alikuwa ni Peter Cech katika milingoti mitatu wakati doto la  Schweinsteiger kiungo katili  linakula nguzo ya pembeni.

Waandishi wengi pamoja na mashabiki wa timu hasimu tena kutoka Uingereza  walizikosoa na kubeza mbinu za Mwalimu  Di Matteo za kupaki basi. Alipoulizwa alijibu "Tulipaki basi kwenye barabara tulizojenga sisi Kama wanataka wajenge zao alafu watupangie wapi pa kupaki". 

2012 CHELSEA NA UBINGWA WA KWANZA ULAYA NA WA KWANZA KWA JIJI LOTE LA LONDON.

Post a Comment

0 Comments