WACHEZAJI wa kimataifa wa timu za Simba na Yanga Clatous Chama, Fiston Mayele, Kennedy Musonda na Henock Inonga wameondoka leo kwenda kutumikia nchi zao kwenye michuano ya kimataifa inayohusisha timu za Taifa.
Wachezaji hao wamekutana leo kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere, jijini Dar es Salaam. Chama na Musonda wanaelekea Zambia, wakati Mayele na Inonga wao wanakwenda Jamhuri ya kidemokrasia ya Congo (DRC) Congo.
Wachezaji hao wanaenda kuchezea nchi zao katika michuano ya kuwania kufuzu fainali za Afrika (AFCON).
0 Comments