Ticker

7/recent/ticker-posts

BEI YA MAFUTA YA PETROL, DIZELI YAZIDI KUPAA

Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA), imetangaza kupanda kwa bei kikomo za bidhaa za mafuta ya petroli hapa nchini zitakazotumika kuanzia leo Jumatano October 04, 2023 saa 6:01 usiku ambapo kwa mwezi October 2023, bei za rejareja za mafuta katika Mkoa wa Dar es Salaam petrol ni Tsh. 3281 kwa lita, dizeli Tsh. 3448 na mafuta ya taa 2943.

Mwezi uliopita (Septemba) bei za rejareja za mafuta katika Mkoa wa Dar es Salaam petrol ilikuwa ni Tsh. 3213 kwa lita, dizeli Tsh. 3259 na mafuta ya taa 2943.

Post a Comment

0 Comments